Flickr

Breaking News
recent

Duniani Teknolojia imeziandika headlines tena kwa hiki kifaa kinachofananishwa na gari… (Video)

Kitu kizuri ni kwamba Teknolojia imekuwa ikirahisisha vitu vingi sana sikuhizi… waliobuni hiki kifaa wamekipa jina la ‘Walk Car‘ yani wanakifananisha na gari linalomrahisishia mtu kutembea !!
Huu ni ubunifu wa jamaa toka Japan, kazi imefanywa na jamaa anayeitwa Kuniako Saito akishirikiana na wenzake wa Kampuni ya Cocoa Motors..
Uko ubunifu ulioitangulia hii, ni kile kifaa cha Hoverboard Segway au iohawk japo chenyewe kina changamoto zake.. kina matairi mawili tu, kama huwezi kutembea nacho unaanguka wakati wowote yani !!
hqdefault
WalkCar hiki hapa aisee, kifaa kidogo kabisa kama laptop lakini kinaweza kukutembeza umbali wa Kilometa mpaka 10 kwa saa moja… uzuri mwingine ni kwamba Walk Car ina matairi manne na kinatumia mfumo wa kuchaji kwa umeme.

Kifaa hiki Bei yake inagusa kama Dola 800 ambazo kwa Bongo inakuwa kama Tshs. Milioni 1.7 hivi !!
Unknown

Unknown

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.